Teacher.co.ke
Latest Education News, Free School Notes, and Revision Materials

MASWALI YA MAPAMBAZUKO YA MACHWEO NA HADITHI NYINGINE

MASWALI YA MAPAMBAZUKO YA MACHWEO NA HADITHI NYINGINE

  • FADHILA ZA PUNDA

  1. Kwa kutaja mifano mitano kutoka kwenye hadithi, Eleza ni kwa nini hadithi hii ikapewa anwani ya “Fadhila za punda”
  2. Fafanua sifa za wahusika wafuatao kama zinavyojitokeza katika hadithi hii
    1. Luka
    2. Lilia
    3. Babake Lilia
  3. Jadili nafasi ya mwanamke katika hadithi hii
  4. Eleza Dhamira ya mwandishi wa hadithi hii
  5. Taja na ueleze umuhimu za tamathali zozote Nne za lugha zilitotumika katika hadithi hii.
  • MSIBA WA KUJITAKIA

  1. Jadili maudhui yoyote matatu yanayojitokeza katika hadithi hii
  2. Jadili mbinu zozote nne za kimtindo zilizotumika katika hadithi hii
  3. Eleza sifa na umuhimu wa wahusika wafuatayo
    1. Sugu Junior
    2. Machoka
    3. Zuhura
  4. Eleza kikamilifu ni kwa nini jimbo la matopeni halijahuhudia maendeleo ya kisiasa tangu nchi kupata uhuru
  • MAPAMBAZUKO YA MCHWEO

  1. Jadili ufaafu wa anwani Mapambazuko ya Mchweo
  2. Eleza maudhui makuu ya hadithi hii
  3. “….siyo Yule wa kujishaua mbele zako huku akifisidi rasilmali ya Nchi …..”
    1. Eleza muktadha wa dondoo
    2. Jadili jinsi wahusika mbalimbali wanazaofisidi rasilmali ya nchi katika hadithi hii
    3. Taja na ueleze tamathali ya usemi iliyotumika katika dondo hii
  4. Eleza changamoto za ukosefu wa ajira kama zinavyojitokeza katika hadithi hii
  • HARUBU YA MAISHA

  1. Eleza kwa ufupi hadithi hii inahusu nini?

    “Naja, nakamilisha shughuli ndogo hapa kisha nianze safari……”

    1. Weka dondoo hili katika muktadha wake
    2. Eleza sifa za msemaji wa kauli hii
  2. Jadili changamoto wanazokumbana nazo waajiriwa kwa kurejelea hadithi hii
  3. Jadili umihimu wa matumizi ya dayalojia katika hadithi hii.
  • SABINA

  1. Eleza matatizo yanayomkumba mtoto wa kike kwa mujibu wa hadithi hii
  2. Je, unajifunza nini kutokana na hadithi hii
  3. Jadili mbinu tatu za lugha zilizotumiwa katika hadithi hii
  • MZIMU ZA KIPWERERE

  1. Eleza ni kwa nini mzimu wa kipwerere uliogopwa sana
  2. Jadili matumizi ya kinaya katika hadithi hii
  3. Eleza sifa za wahusika wafuatao kama zinavyodhihirika katika hadithi hii
    1. Msimulizi
    2. Bishoo
    3. Salihina
  4. Je unajifunza nini kutokana na hadithi hii.
  • KILA MCHEZEA WEMBE

  1. Unafikiri ni kwa nini msimulizi amechagua kutumia barua kusimulia kisa chake
  2. “ondoa wasi wasi mhibaka, you are in safe hands. Usiulize maswali its okey.tulikuja sote jana baada ya dance, umesahau hivi?”
    1. Fafanua muktadha wa dondoo hili
    2. Taja na ueleze mbinu za lugha zinazojitokeza katika dondoo
  3. Jadili kwa kina madhara katika jamii kama yanavyodhihirika katika hadithi hii
  4. Msiba ya kujitakia hauna kilio
    1. Eleza ukweli wa methali kama unavyojitokeza katika hadithi hii
    2. Taja na ueleze umuhimu wa tamathali nyingine nne za usemi zilizotumiwa katika hadithi hii
  • KIFO CHA SULUHU

  1. Eleza maana mbalimbali za kifo cha suluhu kama zinavyojitokeza katika hadithi hii
  2. Fafanua maana na umuhimu wa tamathali zifuatazo za lugha kama zilivyotumika katika hadithi hii
    1. Methali
    2. Takriri
  3. Jadili matumizi wa barua katika kuendeleza maudhui ya hadithi hii
  4. “kisasi hakifai” jadili hoja hii kwa kukita hoja zako kwenye matukio ya hadithi hii
  • AHADI NI DENI

  1. Jadili ufaafu wa anwani Ahadi ni deni katika hadithi hii
  2. Jadili umuhimu wa elimu kwa mototo wa kike kulingana na hadithi hii
  3. Eleza maana ya maudhui ya taasubi ya kiume yalivyoshughulikiwa katika hadithi hii
  • TOBA YA KALIA

  1. Unafikiri ni kwa nini hadi hii umepewa kichwa cha toba ya kalia?
  2. Jadili hasara ya ufisadi kwa kuzinngatia hadithi hii
  3. Eleza matumizi ya mbinu rejehi katika hadith hii
  4. Ukweli ndio mwanzo wa kupona kwa majeraha ya jadi! Jadili ukweli wa kauli hii kwa mujibu wa hadithi hii
  • NIPE NAFASI

  1. Eleza tafsiri tano ya kichwa cha hadithi hii ” Nipe Nafasi”
  2. Jadili matatizo yanayomkumba mwanamke katika jamii kwa mujibu wa hadithi hii
  3. Eleza ni kwa kiwango gani unakubaliana au kutokubaliana na mawazo ya wahusika wanaume kuhusu nafasi ya mwanamke katika hadithi hii.
  4. Unafikiri ni kwa nini mwandishi aliamua kutumia motto kusimulia hadithi hii
  5. Jadili mbinu zozote tano za kimtindo zilizotumiwa katika hadithi hii
  • NILITAMANI

  1. Taja vitu sita ambayo msimuliza anavitamani maishani
  2. ” tama mbele mauti nyuma” jadili ukweli wa kauli hii kwa kurejelea hadithi hii
  3. Unajifunza nini kutokana na hadithi hii
  • POPA

  1. Mwandishi wa hadithi hii anawatahadharisha watu dhidi kuwa na pupa maishani dhibitisha
  2. Umaskini umekuwa janga katika nchi nyingi zinazoendelea. Jadili kwa kurejelea hadithi hii
  3. Jadili maovu yanayoutendeka katika hadithi hii.
  4. Jadili matumizi ya mbinu ya majazi katika hadithi hii
  5. Hadithi hii inahishia katika taharuki. fafanua


Comments are closed.

CHECK DOMAIN